December 10, 2013





SEIF Ahmed ‘Magari’ ametangazwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Michuano ya Kimataofa.
 
Magari ambaye amekuwa jembe la Yanga katika usajili kwa kuwa ni mjumbe wa kamati ya usajili, ametangazwa leo na Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji.
Manji amesema Magari atafanya kazi ya kuteua wajumbe ambao wataunda jopo la kamati yake hiyo.
“Magari atakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Michuano ya Kimataifa ambaye hapo baadaye atawataja wajumbe atakaokuwa nao kwenye kamati yake hiyo,” alisema Manji.
Kupitia kamati hiyo, Magari ataongoza kazi ya kuratibu zoezi zima la maandalizi katika mechi za kimataifa za Yanga.
Yanga ndiyo wawakilishi wa Tanzania katika michuano mikubwa ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic