December 10, 2013


Timu ya Tanzania Bara imeshindwa kufika fainali baada ya kuchapwa bao 1-0 na wenyeji Harambee Stars.


Katika mechi iliyokuwa inapigwa kwenye Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi na Kili Stars kushindwa kufurukuta.
Bao la Clifton Miheso katika dakika ya 4 baada ya kipa Ivo Mapunda kuupangua mpira, liliizamisha Stars ambayo haikucheza vizuri.
Juhudi za Stars kusawazisha bao hilo bila ya mafanikio huku safu yake ya ulinzi ikihaha kuwazuia Miheso na Allan Wanga.

Kutokana na ushindi huo, Kenya sasa itaivaa Sudan na Stars itaivaa Zambia kwa mara ya pili kutafuta mshindi wa tatu, mechi zitapigwa Alhamisi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic