December 11, 2013




Manchester United imefanikiwa kuichapa Shaktar kwa bao 1-0 katika mechi ya Ligi ya mabingwa Ulaya.
 
Bao la United limetupiwa kimiani Phil Jones lakini kali zaidi ni Man City kuichapa Bayern Munich 3-2 ikiwa kwao Munich, Ujerumani.




Ingawa Bayern walitangulia lakini City walizinduka na kusawazisha mabao yao kupitia David Silva, Kilarov na James Milner akamaliza kazi.

Cristiano Ronaldo naye amerejea uwanjani na kusaidia Real Madrid kuichapa Copenhagen kwao kwa mabao 2-0, yeye akifunga la pili lakini Luka Modric ndiye alifungua mlango kwa bao la kwanza.


Dakika ya 89, Ronaldo angeweza kufunga bao la pili la mkwaju wa penalti aliopiga haukuzaa bao.
Matokeo mengine:

PSG walilala kwa mabao 2-1 kutoka kwa wenyeji wao Benfica licha ya kutangulia na bao la Cavani. Vicktoria Plzen 2-CCSKA 1, Real Sociedad 0, Bayer Leverkusen 1.




Mechi kati ya Galatasaray dhidi ya Juventus imeahirishwa kutokana na barafu kujaa uwanjani.
Juhudi za kuziondoa barafu hizo hazikuzaa matunda na mwisho ikatangazwa kuahirishwa kwa mechi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic