December 11, 2013





Wachezaji saba raia wa Nigeria juzi walitua kwenye mazoezi ya Ashanti United yanayofanyika kwenye Uwanja wa Msimbazi Rover, Ilala, Dar, kwa nia ya kusajiliwa klabuni hapo.
 
Wanigeria hao waliungana na wachezaji wengine ambao nao kwa mara ya kwanza wanafanya mazoezi na timu hiyo yenye maskani yake maeneo ya Ilala jijini Dar ambao ni wachezaji wawili wa zamani wa Simba, Juma Jabu na Mohammed Banka, walio kwenye mazungumzo na timu hiyo.

Mara baada ya kuisha kwa mazoezi hayo yanayofanyika majira ya jioni hivi.
Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Nico Kiondo, alisema wageni hao hawana nafasi klabuni hapo kutokana na viwango vyao duni.
“Ni wachezaji wenye viwango vya kawaida sana, hatuna haja ya kuwachukua kwa sababu hapa nyumbani tuna wachezaji wenye viwango vizuri zaidi yao na sidhani kama watakuja tena, nafikiri Kocha Kibadeni (Abdallah) ameshazungumza nao juu ya viwango vyao ukilinganisha na watu tunaowahitaji.
“Lakini Banka na Jabu bado tunaendelea kuwaangalia tukiwa bado tunazungumza nao kwa ajili ya mzunguko wa pili” alisema Kiondo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic