Kocha Mkuu wa timu ya taifa
ya Uganda, The Cranes, Sredojevic Milutin ‘Micho’ amesema Moses Oloya au
Emmanuel Okwi wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa Yanga hasa katika Ligi ya Mabingwa afrika.
Kumekuwa na taarifa kuwa Yanga imekuwa ikiwafuatilia Waganda hao huku ikitaka kumchukua mmoja wao kutokana na mazungumzo yao yatakavyokuwa.
Akizungumza na SALEHJEMBE,
Micho alisema wachezaji hao wawili wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa aina ya
uchezaji wa Yanga.
“Nimeona Yanga inacheza kwa
kasi, pia mabeki wanapita au mawinga wanapiga krosi.
“Ukiwa na wachezaji kama
Okwi au Oloya kwa mfumo huo, msaada unakuwa mkubwa sana.
“Kweli nimesikia
wanawafuatilia na iwapo wakimpata mmoja wao, basi watakuwa msaada kwao,”
alisema.
Kuhusiana na kuvuliwa
ubingwa na Tanzania Bara, Micho alisema The Cranes hawakuwa makini.
“Tulipoteza nafasi nyingi na
kufanya uzembe kwenye safu ya ulinzi. Mwisho tulistahili adhabu,” alisema.
Kili Stars iliing’oa Uganda
kwa mikwaju ya penalti 3-2 ikiwa ni baada ya sare ya mabao 2-2 katika mechi ya
robo fainali ya michuano ya Chalenji.









0 COMMENTS:
Post a Comment