Uongozi wa Simba umempa nyumba kipa mpya
wa timu hiyo, Yaw Berko, maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam kwa ajili ya
kukaa katika muda wote atakaoitumikia klabu hiyo.
Berko ambaye yupo nchini kwa sasa,
amemalizana na uongozi wa klabu hiyo na leo Jumatatu anatarajiwa kusaini
mkataba wa miezi sita kwa ajili ya kuitumikia katika mzunguko wa pili wa ligi
kuu baada ya kuondolewa kwa Abel Dhaira.
Kikizungumza na Championi Jumatatu,
chanzo cha habari cha kuaminika kutoka Simba, kimesema Berko atakwenda kukaa
Sinza kwenye nyumba ambayo ni maalum kwa wachezaji hadi mkataba wake
utakapoisha.
“Kuhusu suala la nyumba ama sehemu ya
kukaa Berko, haina shida kwani Simba ina nyumba nyingi ambazo huwa tunawaweka
wachezaji wetu, hivyo na yeye atapewa nyumba mojawapo kati ya hizo.
“Kwa sasa yupo kwenye mazungumzo ya
mwisho na uongozi ya kuingia mkataba mpya kwani ametua ili kumalizana na
uongozi kisha atarudi kwao na baadaye atarejea tena kuanza kazi,” kilisema
chanzo hicho.
SOURCE: CHAMPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment