January 10, 2014



 
MICHAEL AKIMDHIBITI MWOMBEKI WA SIMBA
Yule beki mrefu wa Ruvu Shooting, George Michael ambaye alijizolea umaarufu kwa kuwasimamisha mastraika wa Simba na Yanga katika raundi ya kwanza Ligi Kuu Bara, amevunjika mguu na imeelezwa huenda akakosa mzunguko wote wa pili.


Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire amesema Michael alivunjika mguu wakati wa mazoezi ya timu hiyo juzi Jumatano kwenye Uwanja wa Mlandizi, hali aliyosema ni pigo kubwa, hususan timu yao itapokutana na vigogo raundi ya pili.

Beki huyo ndiye pia aliyempa wakati mgumu Amissi Tambwe wa Simba wakati timu hizo zilipokutana.

“Alikuwa katika harakati za kukaba, huenda akawa nje kwa muda mrefu zaidi. Bado hatutajua ni lini atarejea maana hajapata vipimo na alitarajiwa kupimwa Alhamisi (jana), lakini uhakika nilionao ni kwamba tutamkosa raundi ya pili yote,” alisema Bwire.

Wakati huohuo alisema leo kikosi chao kitakuwa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Friends Rangers kwa ajili ya kujiandaa na raundi ya pili itakayoanza kutimua vumbi Januari 25.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic