January 24, 2014



 
CHOLLO AKIWA KAZINI
Nahodha na beki wa pembeni wa Simba, Said Nassor ‘Chollo’, leo Ijumaa anatarajia kupelekwa kwenye Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa kiafya, hivyo kuenguliwa kwenye kikosi kitakachoivaa Rhino Rangers ya Tabora, keshokutwa Jumapili.


Chollo aliyerejea hivi karibuni baada ya kukaa nje kwa muda kutokana na maumivu ya nyama za paja za mguu wa kulia, amepata maumivu mapya ya nyonga juzi alipokuwa mazoezini.

Daktari wa Simba, Yassin Gembe amesema kuwa kutokana na maumivu makali aliyokuwa nayo beki huyo pamoja na kuumia kwake mfululizo katika siku za hivi karibuni, wameamua kumfanyia vipimo vya kina vya mwili mzima kujua undani wa majeraha yake hayo ya mara kwa mara.

“Chollo ataikosa mechi ya Rhino kutokana na maumivu ya nyonga aliyokuwa nayo na Ijumaa (leo) tutampeleka MOI kwa ajili ya vipimo vya kina kujua nini chanzo cha kuwa majeruhi mara kwa mara,” alisema Gembe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic