January 24, 2014



 
COASTAL WAKIWA KAZINI DHIDI YA YANGA
Uongozi wa Coastal Union umekataa tiketi za elektroniki kutumika kwenye Uwanja wa Mkwakwani kwa kuwa hakuna kati yao anayejua matumizi ya teknolojia hiyo.


Uwanja wa Mkwakwani uliopo Tanga ambao unatumiwa na Mgambo na Coastal, ni miongoni mwa viwanja ambavyo vimefungwa mashine za kielektroniki.

Katibu Mkuu wa Coastal, Kasim El Siagi amesema uwanja huo haujawa tayari kwa matumizi ya teknolojia hiyo licha ya ujenzi wa mashine hizo kuwekwa kwenye milango miwili kati ya mitano iliyopo uwanjani hapo.

“Hakuna semina yoyote iliyotolewa juu ya matumizi ya mashine hizo, tujiulize mamia wanaotumia lango kuu wanafanyaje na milango yao haijawekwa mashine? Mpaka sasa meneja wa uwanja hajui na hata hao CRDB wapo kimya.

“Tunaomba mpango huu uachwe mpaka tucheze mechi mbili (dhidi ya Oljoro na Yanga) kisha vikao vya wadau hapa Tanga vifanyike watu waelimishwe,” alisema El Siagi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic