January 28, 2014


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm amesema baada ya mechi tatu, kikosi chake kitaimarika zaidi.


Van Der Pluijm, raia wa Uholanzi amesema amebahatika kukaa na kikosi hicho kwa wiki moja tu akifanya nao kazi na ameona kuna wachezaji wengi wenye vipaji lakini anahitaji muda kidogo.
“Kweli nahitaji muda kidogo, lakini hauwezi kuwa muda mrefu sana. Tutakuwa katika hali nzuri zaidi ya sasa pia kuna mabadiliko kadhaa nitakuwa nimefanya,” alisema.
Kocha huyo aliyewahi kufundisha soka nchini Ghana, amesema baada ya mechi tatu, atakuwa na uhakika wa nini atafanya katika kikosi hicho kwa kuwa tokea ameanza si muda mrefu.

Mechi yake ya kwanza ya mashindano ilikuwa ni pale Yanga ilipovaa Ashanti United katika mechi ya kwanza ya mzunguko wa pili na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 ingawa haikunyesha soka la kuvutia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic