January 28, 2014


Na Mwandishi Wetu, Tanga
Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga wameuchangamsha mji wa Tanga kutokana na mechi ya kesho kuwa gumzo.


Pamoja na mashabiki wa Coastal Union kujiamini kwamba kesho lazima Yanga ikae, lakini Yanga wanaonekana kujiamini zaidi.
Katika sehemu mbalimbali za mji wa Tanga, gumzo kubwa limekuwa ni namna mechi hiyo ya kesho itakavyokuwa.

Yanga tayari iko mjini hapa na imefanya mazoezi huku ikionyesha kikosi chao kipo fiti na wanaisubiri Coastal kwa hamu.

Gumzo la Uturuki na Oman ambako timu hizo ziliweka kambi pia limechukua nafasi kubwa.

Timu hizo mbili zote ziliweka kambi nje ya nchi, Yanga ilisafiri hadi Uturuki, Coastal ikajificha nchini Oman kujiandaa na Ligi Kuu Bara.
Yanga imeanza Ligi Kuu Bara mzunguko wa pili kwa ushindi wa mabao 2-1 wakati Coastal Union ilishikiliwa na JKT Oljoro ikiwa kwake Mkwakwani.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic