January 23, 2014


Taarifa za Emmanuel Okwi kuzuiwa kuichezea Yanga zilikuwa furaha kubwa kwa mashabiki wa Simba waliojitokeza katika mazoezi ya timu yao juzi kwenye Uwanja wa Kinesi jijini Dar.


Okwi ambaye yupo Yanga, amezuiwa kuichezea timu hiyo na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana na kuwa na kesi tatu tofauti juu ya uhamisho wake kutoka Simba kwenda Etoile ya Tunisia, kisha kusajiliwa SC Villa ya Uganda na baadaye kutua Yanga.

SALEHJEMBE iliwashuhudia mashabiki hao wakiimba kwa sauti kubwa ‘Okwi! Okwi! Okwi!’ Huku mazoezi ya Simba yakiendelea, hali iliyozua taharuki kwa wengine ambao hawakuwa na taarifa.


“Muacheni akutane na rungu la Fifa si anajifanya anajua sana! Tatizo wachezaji wetu wa Kiafrika wanapenda sana hela za papo kwa papo, sasa zitamtokea puani,” alisikika shabiki mmoja huku akiungwa mkono na wengine wengi waliokuwa wakitoa maneno ya kejeli kwa Yanga na Okwi aliyekuwa mchezaji wa Simba.

Kamati ya Hadhi ya Wachezaji ya TFF, imesimamisha usajili wa Okwi hadi hapo itakapopata ufafanuzi kutoka Fifa.

Tayari suala lake limeanza kushughulikiwa na maana yake atakosa mechi ya Jumamosi dhidi ya Ashanti.

Okwi anawasili nchini kesho alfajiri akiwa na kikosi cha Yanga kilichokuwa kimeweka kambi nchini Uturuki.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic