January 23, 2014

Wakala wa Wayne Rooney leo amefanya mazungumzo na uongozi wa Manchester United kuhusiana na kubaki kwa mchezaji huyo.

MAzungumzo kati ya Paul Stretford ambaye ni wakala wa Rooney au Wazza na bosi, Ed Woodward yalikuwa ni kujadili kuongeza mkataba ambao umebaki miezi 18.
 
WAKALA AKIWASILI OLD TRAFFORD LEO
Imeelezwa Man United imeshituka na kuona ijadili mkataba mapema kwa kuwa Rooney anaonekana kuanza kuvutiwa na Chelsea pamoja na Real Madrid ambazo zimeonyesha nia ya kumnasa.



Bado haijajulikana hasa mwafaka waliofikia na nini kinachotakiwa lakini inaonekana Man United imepania kumbakiza Wazza kwa muda mrefu zaidi

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic