January 10, 2014





Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons, David Mwamwaja, ameongeza kasi ya mazoezi ambapo sasa watafanya mara tatu kwa siku, ikiwa ni mkakati wa kujiweka fiti kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara.


Kocha huyo amesema mazoezi yatakuwa yakifanyika mara tatu kwa siku ambapo ni asubuhi, mchana na jioni.

"Nafurahi kuona Peter Michael ameanza kufanya mazoezi na anaendelea vizuri kwani alikuwa anaumwa ila kwa sasa hali yake imetengemaa na anafanya vizuri, nina imani ataendelea kufanya vizuri kama msimu uliopita.

"Timu yangu inacheza kwa kutegemeana, hatutegemei mtu mmoja, wachezaji wanaonyesha kuelewa mazoezi yangu, hiyo inanipa moyo wa kufanya vizuri ligi itakapoanza,” alisema Mwamwaja.

Prisons inashika nafasi ya pili kutoka chini katika msimamo wa ligi kuu, ambapo imeshinda mechi moja, sare sita na kufungwa sita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic