February 26, 2014

SWITA AKIMDHIBITI MESSI WA SIMBA

Kiungo mchezeshaji wa JKT Ruvu aliyefunga mabao mawili na kuiangamiza Simba Jumapili iliyopita, Emmanuel Swita, amesema yupo tayari kurejea Yanga iwapo watamhitaji.

Kiungo huyo alicheza Yanga msimu wa 2007/2008 kabla ya kutolewa kwa mkopo kwenda Toto African hadi mkataba wake ulipokwisha.

Swita alisema wakati anaondoka Yanga hakuondoka kwa ubaya bali alitolewa kwa mkopo na alishangaa kuona wapo kimya hivyo kuchukua hamsini zake, lakini sasa anatamani kurudi.
 “Nashukuru kwa kufunga mabao hayo, najua Simba walidhani labda sisi kufungwa mabao sita na Prisons ni wepesi, kumbe tulikuwa tumechoka tu.

“Lakini mimi kama kuna timu inanitaka, hata kama ni Yanga nipo tayari kujiunga nayo, sina kinyongo,” alisema Swita. 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic