February 26, 2014


Bekiwa zamani wa Yanga, Stephano Mwasyika, anayechezea Ruvu Shooting kwa sasa amesema mabao ya haraka yaliwatoa mchezoni na kujikuta wakipokea kipigo kikubwa cha mabao 7-0 kutoka kwa Yanga.


Ruvu walikula kichapo hicho kwenye mchezo mkali wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumamosi iliyopita.

Ruvu ilijikuta ikifungwa bao la kwanza sekunde 58 ya mchezo kipindi cha kwanza, bao lililofungwa  na Didier Kavumbagu huku bao la pili likifungwa dakika 2 na winga Simon Msuva.

Mwasyika amesema kuwa licha ya kufanya maandalizi  hawakutarajia kufungwa mabao ya mapema kiasi kile kutokana na uzuri wa timu yao.
“Yale mabao tuliyofungwa mwanzoni ndiyo yalitutoa mchezoni, hatukutegemea kabisa kuruhusu mabao yale ila wapinzani walitumia udhaifu wetu uliojitokeza na kuweza kutufunga, malengo yalikuwa kushinda mchezo ule (Jumamosi).

“Tulijaribu kujipanga lakini ilishindikana, wenzetu walionekana wakitumia mipira mirefu ambayo wameweza kuimudu vema kuliko sisi ila tunaenda kujipanga na mchezo unaofuata  tusipoteze kama huu,” alisema Mwasyika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic