February 26, 2014


Katika kuhakikisha inafanya maandalizi mazuri na yenye ubora kwa ajili ya kuikabili Al Ahly ya Misri kwenye mchezo wa Klabu Bingwa Afrika, timu ya Yanga imeamua kuweka kambi kwenye hoteli ambayo mara ya mwisho ilitumiwa na timu ya taifa ya Ivory Coast.

Yanga ipo Ledger Hotel, Kunduchi jijini , Dar, iliyotumiwa na Ivory Coast iliyokuja na mastaa kibao kama Yaya Toure, Salomon Kalou, Wilfried Bony na Gervinho.

Ivory Coast walikaa hapo wakati wakiwa hapa nchini ajili ya mechi ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia ilipovaana na Taifa Stars na kushinda 4-2.

Yanga imeanza kambi hiyo jana na itadumu hapo mpaka Ijumaa, ambapo Jumamosi asubuhi wanatarajiwa kurejea katikati ya jiji tayari kuwakabili Al Ahly, mabingwa watetezi wa mashindano hayo.
Pamoja na hayo Yanga itakuwa ikifanya mazoezi yake kwenye Uwanja wa kisasa wa Boko uliopo Boko nje kidogo ya Dar es Salaam, ikiwa ni kilomita chache kutoka hoteli walipoweka kambi yao.


Hata hivyo, kocha mkuu wa Yanga, Mholanzi Hans van Der Pluijm amesema kuwa ameukubali ubora na uzuri wa uwanja huo na kutamani kuendelea kukifundisha kikosi chake mpaka mwisho wa msimu huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic