February 14, 2014





Benchi la ufundi la Mbeya City limesema kuwa limejipanga vilivyo kuhakikisha kiungo mshambuliaji wa Simba, Ramadhani Singano ‘Messi’ hafurukuti katika mechi ya kesho ya Ligi Kuu Bara itakayozikutanisha timu hizo kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya kwa kumwekea ulinzi wa kutosha.


Kocha mkuu wa timu hiyo, Juma Mwambusi amesema kikosi chake kipo vizuri kwa mchezo huo na mipango ya kuwadhibiti wasumbufu imekamilika.

“Tumejipanga vizuri kwa mechi hiyo na ni matumaini yetu kuwa tutaibuka na pointi tatu ambazo zitatusaidia kujiweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi hii.

“Kuhusiana na Messi ni mchezaji mzuri lakini tayari nimeshawapa majukumu vijana wangu, endapo watafanikiwa kumdhibiti kama tulivyopanga tutaibuka na ushindi, kwani yeye hivi sasa ndiye mpishi mkubwa wa mabao ya Simba,” alisema Mwambusi.

Aidha, Mwambusi aliongeza kuwa hali ya mvua kunyesha mara kwa mara ilisababisha kukosa muda mzuri wa kufanya mazoezi lakini hiyo haiwezi kuvuruga mipango yake ya ushindi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic