February 28, 2014



KIKOSI cha Al Ahly ya Misri, kilianza rasmi mazoezini jijini juzi Alhamisi  ikiwa ni siku moja tu baada ya kuwasili nchini kikitokea kwao Cairo, Misri.

Mazoezi ya mabingwa hao wa Afrika yalikuwa yakifanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Kimataifa ya Tanganyika (IST) iliyopo Upanga.

Lakini kama ilivyo ada, timu za Misri zinapokuwa nchini zimekuwa na uoga wa hujuma, hivyo ilikuwa ni ‘full’ vituko.
Ulinzi ulikuwa mkali kupita kiasi katika eneo linalozunguka shule hiyo, kwani Al Ahly iliwasili mazoezini hapo ikiwa kwenye msafara unaongozwa na pikipiki ya askari wa barabarani inayopiga king’ora.

Lakini uwanjani hapo, walinzi walikuwa wakizunguka kila eneo la uwanja huo na maeneo mengine ya shule hiyo ili kuhakikisha hakuna mtu yeyote anayepata upenyo wa kushudia mazoezi ya timu hiyo, lakini Championi likawapiga bao, likashuhudia na kupata picha.


Waandishi na wapigapicha wa gazeti hili walikumbana na wakati mgumu kutoka kwa walinzi hao katika siku zote mbili walizofuatilia mazoezi ya Al Ahly.
Katika siku ya kwanza, Jumatano iliyopita, baada ya kufika shuleni hapo kwa lengo la kutaka  habari  pamoja na picha za mazoezi ya timu hiyo wandishi wa gaezeti hili walizuiliwa na walinzi wa shule hiyo.

Walinzi hao waliokuwa wamesimamiwa na jamaa mmoja ambaye alionekana kama ofisa wa ubalozi wa Misri hapa nchini walisema kuwa wamekatazwa na viongozi wao kuwa mtu yoyote ambaye si hatakiwi kuingia ndani ya uzio wa shule hiyo.

Baada ya kujadiliana kwa muda mrefu kati ya walinzi hao na wandishi wa gazeti hili walikuja walinzi wengine na kuwataka waondoke katika ene hilo.
“Tunaomba mwondoke katika eneo hili kwani hamruhusiwi kuwa hapa nuda huu na tunawaomba msipoteza muda wenu hapa hamuna yoyote atakayepata nafasi ya kushudia mazoezi haya hata kwa dawa,” alisema mmoja wa walinzi hao huku wengine wakiwa wamenuna bila hata ya kuonyesha meno yao.
 Baada ya hali hiyo, waandishi wakajipanga na kuzunguka nyuma ya uzio ambako kulikuwa na upenyo kidogo, wakapanga mawe na kuanza kushuhudia mazoezi hayo.
Ili kupata picha safi zaidi, zoezi la kupanga mawe haraka lilifanyika na picha ambazo ni exclusive zikapigwa “ta ta ta”, kama unavyoziona kwenye ukurasa huu.
Jumatano:
Kikosi hicho cha Al Ahly kilifika uwanjani hapo Saa 9.30 Alasiri kikiwa na msafara wa magari sita moja likiwa ni basi, Kakore Trans lilokuwa limebeba wachezaji. Magari madogo yalikuwa yamewachukua makocha na maofisa wa ubalozi wa Misri nchini.
Rasmi walianza mazoezi Saa 9.40 Alasiri kwa wachezaji wa timu hiyo kuzunguka nusu uwanja mara 10 kisha wakanyosha viungo na kuanza kuchezea mpira kwa kupigana pasi fupi fupi kwa muda wa dakika 15.
Baada ya hapo walibadili programu na kuanza kurushiana mpira kama wanacheza Rugby kwa muda wa dakika 15. Wakanyoosha viungo kisha wakanza kuruka koni.
Baada ya mazoezi hayo walinyosha tena viungo na wakagawanya katika makundi mawili kisha wakanza kucheza mpira na baada ya kumaliza mazoezi yao walikusanyika pamoja na kuomba dua, wakaondoka zao.
Alhamisi:
Ulinzi ulikuwa wa hali ya juu zaidi ya ule wa Jumatano, kwani walinzi walitawanyika semu mbalimbali za uwanja huo kuhakikisha hakuna mtu yeyote anapata nafasi ya kushudia mazoezi hayo.
Hata ule upenyo ambao wandishi wa gazeti hili waliutumia kupata picha pamoja kuona mazoezi ya timu hiyo Jumatano,  ulikuwa umezibwa kwa na kuwekwa mlinzi.
Lakini pamoja na hali hiyo wandishi wa gaezti hili hawakukata tamaa, walendelea kupambana na kunawakati walijifanya kuwa ni maofisa wa Shirikiho la Soka Tanzania (TFF), lakini mambo yalikuwa magumu kwao.
Walinzi waliendelea kuweka ‘uso mbuzi’ na kudai kuwa kama wangewaruhusu kuingia basi kazi zao ‘zingeota nyasi’ kwani kila kitu walichokuwa wakikifanya kilionekana kwenye kamera maalum za ulinzi katika eneo hilo.
Juhudi za kusaka upenyo mwingine zilianza, ukapatikana na kama kawa, picha zikapigwa tena na Championi kikawa chombo pekee kilichopata picha zao mara mbili kwa siku mbili.
Katika mazoezi hayo Alhamisi, wachezaji wa Al Ahly mara baada ya kufika uwanjani hapo, walianza kwa kupasha misuli kisha kuzunguka uwanja mara sita na baada ya hapo walianza kuchezea mpira na wakati huo viongozi wa benchi lao la ufundi wakijadiliana jambo.
 Baada ya hapo waligawanywa katika makundi mawili na kuanza kucheza soka  kwa ushindani wa hali ya juu na kocha wa timu hiyo alikuwa ikiandika kila kitu kilichokuwa kikitokea uwanjani hapo.

Kunawakati walikuwa wakicheza soka la pasi fupifupi lakini kunawakati walikuwa wakicheza pesi ndefu na wachezaji wa timu moja katika mazoezi hayo walionekana kuwa wazuri kwa mpira hiyo.
Hata hivyo baada ya mazoezi hayo yalioanza Saa 10:00 jioni na kumalizi Saa 11:30 walikusanyika na kuomba duwa kisha wakaondoka zao.


SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic