March 1, 2014


Yanga imesema haitahama njia kuu kuepuka michepuko, hivyo imebaki njia kuu na kuweka rekodi mpya kwa kuifunga Al Ahly ya Misri kwa bao 1-0.

Kabla Yanga haikuwa imewahi kuishinda Al Ahly ambao sasa ni mabingwa wa Afrika.

Bao pekee la Nadir Haroub Canavaro katika dakika ya 83, lilimaliza ndoto za Warabu hao wa Misri kunyanyasa kila wanapokuwa Tanzania.

Mechi ilikuwa safi na kila timu ilicheza kwa kujituma, lakini Yanga walipoteza nafasi nyingi za wazi za kufunga.









0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic