February 1, 2014


Kocha maarufu wa Hispania, Luis Aragonés amefariki dunia leo alfajiri akiwa na umri wa miaka 75.


Aragone maarufu kama 'The Wise Man of Hortaleza', mchezaji wa zamani na kocha wa timu ya taifa ya Hispania alikuwa na sifa ya ubaguzi.
Kocha huyo aliwahi kumbagua Thierry Henry na kusababisha apewe adhabu na Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa).
Aliifundisha Hispania tokea mwaka 2004 hadi 2008.
Mwaka 2008, Hispania ilibeba ubingwa wa Ulaya ikiwa mikononi mwake na baada ya hapo, miaka ya Hispania kuchukua makombe ikaanza.

Kwani mwaka 2010, Vicente del Bosque akachukua Kombe la Dunia na 2012 akarudia kutwaa tena Kombe la Ulaya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic