February 11, 2014





Kocha Mkuu wa AS Cannes, Jean Marc Pilorget amesema zimebaki siku chache sana kama hajachoshwa na Shomari Kapombe.
 
Pilorget amesema alivutiwa sana na uwezo wa Mtanzaia huyo, lakini kinachotokea sasa kinamkera.
 
PILORGET
“Nimekuwa nikiuliza kila mara kuhusiana naye kama kweli atakuja huku lini, naambiwa ni kesho na imekuwa hivyo kila siku.
“Mambo yanavyokwenda inaonekana mchezaji pia ana matatizo, nitakuwa na subira kidogo tu.

“Sifurahishwi na mambo yanavyokwenda na kama ikizidi hali hii, nitaangalia mipango mingine,” alisema.

Taarifa zinaeleza Kapombe amelipwa kila anachodai na klabu hiyo lakini uamuzi wake umekuwa ni kubaki jijini Dar.

Wakati uongozi wa AS Cannes inayoshiriki daraja la nne, umekuwa ukitaka arejee kazini mara moja .

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic