February 11, 2014





Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amekubali kuwa Mgambo JKT waliwapoteza katika mechi yao iliyopita.


Logarusic raia wa Croatia amesema Mgambo JKT walistahili kushinda mechi hiyo ya juzi kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga kwa kuwa walicheza vizuri.

“Walicheza vizuri sana, kwa kiwango chetu hatukufanya vizuri katika mechi hiyo.

“Tumeliona hilo na tunaendelea na maandalizi kuhakikisha tunafanya vizuri katika mechi zinazofuatia,” alisema.

Simba imepoteza mechi ya kwanza ya ligi ikiwa chini ya Logarusic baada ya kufungwa na Mgambo bao 1-0.
Katika mzunguko wa kwanza, Mgambo ilicharazwa na Simba kwa mabao 6-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar huku Mrundi, Amissi Tambwe akiingia nyavuni mara nne.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic