February 11, 2014





Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema wanawasubiri Simba kwa hamu.


Mwambusi amesema anawasubiri kwa hamu katika mechi ya Ligi Kuu Bara itakayopigwa Jumamosi  ijayo mjini Mbeya.

Simba itakuwa mgeni wa Mbeya City ambao wamepoteza mechi moja tu kwenye Ligi Kuu Bara baada ya kufungwa bao 1-0 na Yanga.

“Tunajua mechi itakuwa ngumu, Simba watakuwa wamepania kutuangusha lakini kweli sisi tunasubiri kwa hamu.

“Tutaendelea kujiandaa na kikubwa tunachotaka ni kushinda na mwisho ikiwezekana kutwaa ubingwa au kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya kimataifa,” alisema Mwambusi.

Mbeya City ambayo haijafungwa kwenye Uwanja wa Sokoine, ilimaliza mzunguko wa kwanza bila ya kupoteza hata mchezo mmoja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic