February 28, 2014



Mashabiki wa Gor Mahia ya nchini Kenya wamemtumia salamu za rambirambi aliyekuwa kipa wa timu hiyo, Ivo Mapunda, baada ya kufiwa na baba yake mzazi, Philip Mapunda, juzi.


Mauti ya mzazi wa kipa huyo yalitokea Jumanne katika Hospitali ya Ikonda mkoani Njombe na aliwatarajiwa kuzikwa jana Alhamisi katika Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.

Mashabiki wa timu hiyo kupitia mitandao ya jamii wamesema wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kipa huyo kuondokewa na mzazi wake mzee Mapunda ambaye aliugua kwa muda mrefu.

“Tunampa pole sana Mapunda kwa kuondokewa na baba yake tunafahamu yuko katika wakati mgumu sana kwa sasa lakini ni kazi ya Mungu haina makosa bado tunamkumbuka sana huku Kenya kwa kazi kubwa aliyoweza kuifanyia timu yetu,” alisomeka shabiki mmoja.

Ivo ambaye ni kipa wa zamani wa Yanga, amekuwa pia katika wakati mgumu kwenye timu yake ambapo amejikuta akiwekwa benchi katika mechi mbili zilizopita kutokana na kudaiwa kucheza chini ya kiwango.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic