February 28, 2014


Wachezaji wawili wa timu ya taifa ya soka ya wanawake, Twiga Stars inayojiandaa na mchezo wa marudiano dhidi ya Zambia itakayopigwa leo Ijumaa, Chamazi, Dar wameenguliwa kwenye kikosi hicho kutokana na makosa ya utovu wa nidhamu.


Wachezaji hao ambaoni Mwapewa Mtumwana na Flora Kayanda waliondolewa kwenye kambi ya timu hiyo iliyopo kwenye hosteli za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ilala, Dar tangu Jumapili ya wiki iliyopita.

Chanzo makini kutoka ndani ya timu hiyo kimesema, wachezaji hao walienguliwa baada ya kubainika kuwa walitumia kilevi wakiwa bado wapo kambini.

“Waliondoka kwenda kutembea Jumapili, waliporudi jioni walikuwa wamelewa na ilionekana walikunywa pombe nyingi,” kilisema chanzo.


Alipotafutwa Nasra Mohammed ambaye ni kocha msaidizi wa timu hiyo alisema: “Kweli tumewaondoa kutokana na matatizo mbalimbali ya utovu wa nidhamu lakini sitaweza kulizungumzia sana.” 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic