February 28, 2014


Uongozi wa Mbeya City umesema unataka kuhakikisha timu yao inashinda mechi zote za nyumbani zilizosalia katika msimu huu wa Ligi Kuu Bara ambazo ni sawa na pointi 15 ili ifanikiwe kumaliza katika nafasi mbili za juu katika ligi hiyo.


Kauli hiyo ya uongozi wa Mbeya City inamaanisha kuwa kila timu itakayofika kwenye Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya lazima iache pointi zote uwanjani hapo. Timu hizo ni JKT Oljoro, Rhino Rangers, Prisons, Azam FC na Mgambo.

Mwenyekiti wa Mbeya City, Mussa Mapunda amesema wanaelekeza nguvu zao kwa mechi zilizobaki hasa za nyumbani kwa kuhakikisha wanachukua pointi zote.

“Lengo letu kubwa ni kushinda mechi zetu saba zilizobaki katika mzunguko huu wa pili na hatutakuwa tayari kupoteza mchezo hata mmoja hasa katika mechi tano ambazo tutaweza kucheza katika uwanja wa hapa nyumbani.


“Kuhusu suala la ubingwa bado lipo, hatujakata tamaa kabisa tukifanya vizuri kwenye michezo yetu iliyobaki,” alisema Mapunda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic