February 10, 2014


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiq, amewaonya Yanga kutobweteka na ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Komorozine ya Comoro.


Yanga iliibutua Komorozine kwa mabao hayo saba katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, juzi.
Akizungumza mara tu baada ya mechi hiyo, Sadiq alisema Yanga hawapaswi kubweteka na ushindi huo kwa kuwa wanakwenda kucheza ugenini.

“Sasa wanakwenda ugenini, lazima wajiandae vizuri kwa ajili ya mechi ijayo. Hauwezi kujua kwa kuwa mpira una mambo mengi.
“Hawa jamaa wakati fulani walionyesha ushindani, hivyo Yanga wasione wamemaliza kazi, hadi dakika 90 za kule Comoro zikiisha, basi ndiyo watakuwa wamemaliza kazi,” alisema Sadiq aliyeshuhudia mechi hiyo kwa dakika 90.

Yanga inajiandaa kwenda Moroni, Comoro kwenda kuwavaa Komorozine ambao walionyesha kiwango cha chini hiyo juzi na wakivuka wanakutana na mabingwa wa Afrika, Al Ahly.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic