Straika wa Simba, Amissi Tambwe amewajia juu wanaosema kuwa Mbeya City ni timu ngumu
inayosumbua vigogo kwenye Ligi Kuu Bara ambapo amedai kuwa hiyo ni timu ya
kawaida na kuahidi kushinda kesho Jumamosi dhidi ya timu hiyo ya Mbeya.
Tambwe,
raia wa Burundi, amesema timu za Tanzania zinalingana viwango, ndiyo maana hata
wao walifungwa 1-0 na Mgambo JKT ambao wapo mkiani kwenye msimamo.
“Hakuna
timu ambayo inamzidi mwenzake kwa kiwango kikubwa kwenye hii ligi, zote
zinalingana, ndiyo maana zinapishana kwa pointi chache kwenye msimamo,
wanaosema Mbeya City ni ngumu si kweli, isipokuwa wanajitahidi kupata tu
matokeo bora.
“Unaposema
ni timu ngumu au ni kiboko ya vigogo unakosea kwa sababu ukiangalia kiwango
chao ni kama cha timu nyingine tu hapa Tanzania isipokuwa huwa wana
kombinesheni,” alisema Tambwe na kuongeza:
“Nimepanga
nijitahidi kufunga ili kuisaidia timu yangu ishinde lakini najua kila mmoja
atakuwa ananiangalia mimi siku hiyo ili nisifunge, wakumbuke kwamba sipo peke
yangu uwanjani.”
Kwenye
mchezo wa timu hizo uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar zilitoka sare ya
mabao 2-2.
Mbeya
City imefungwa mechi moja katika mechi zote 17 ikiwa inashika nafasi ya tatu
kwenye msimamo huku Simba ikiwa na rekodi ya kupoteza michezo miwili msimu huu
na ipo nafasi ya nne katika msimamo.







0 COMMENTS:
Post a Comment