March 31, 2014

MWOMBEKI KAZINI
Licha ya wachezaji Said Bahanuzi wa Yanga na Betram Mwombeki wa Simba kuonekana si lolote si chochote katika klabu zao, benchi la ufundi la Mtibwa Sugar linaloongozwa na Mecky Maxime, limeonyesha nia ya kuwahitaji wachezaji hao kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Bahanuzi alikuwa akiichezea Mtibwa kabla hajasajiliwa Yanga na sasa timu hiyo ya Morogoro inataka kumrudisha. Mwombeki mwenyewe alianza kwa mbwembwe Simba lakini ameshindwa kupata nafasi chini ya kocha Zdravko Logarusic.

Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime, ameliambia gazeti hili kuwa, endapo atafanikiwa kuwapata wachezaji hao, itakuwa ni jambo zuri kwake kwani ana uhakika kuwa watamfanyia kazi kubwa ambayo itarudisha heshima ya klabu hiyo.
Alisema Simba ya Yanga kwa sasa zinawaona wachezaji hao kuwa hawana lolote lakini yeye anaamini kuwa ni miongoni mwa washambuliaji hatari ambao timu hizo zimeshindwa kujua ni jinsi gani ya kuwatumia.
“Ligi kuu ya msimu huu ndiyo kwanza inafikia ukingoni hivi karibuni na baada ya hapo taratibu za usajili zitaanza, hivyo tutaangalia kama tunaweza kuwasajili.
“Wachezaji hao kwa hakika ni miongoni mwa washambuliaji bora hapa nchini lakini wamenyimwa nafasi, endapo nikiwapata nitawatengeza na kuwarudisha katika viwango vyao ambavyo watu wote walikuwa wakivijua,” alisema Maxime.

Maxime pia amewaonya wachezaji kuwa makini kufanya maamuzi hasa ya kujiunga Simba au Yanga, kwani mara nyingi vipaji vyao hupotea kutokana na kushindwa kutumika vizuri kutokana na uhaba wa nafasi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic