April 25, 2014


Uongozi wa Azam FC umempa kibarua kocha mkuu wa timu hiyo, Joseph Omog, kwenda kusaka wachezaji pindi atakapokuwa mapumziko nchini kwao Cameroon.


Omog alitua Azam wakati wa dirisha dogo la msimu uliomalizika hivi karibuni baada ya kuondoka kwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Stewart Hall aliyemwachia madaraka baada ya uongozi kuona timu hiyo inayumba.

Hata hivyo, baada ya kukabidhiwa majukumu hayo, Omog ameonekana kuitumikia vema timu hiyo na hatimaye kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2013/2014 ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu hiyo tangu ipande daraja.

Katibu Mkuu wa Azam FC, Idrissa Nassoro, amefunguka kuwa, kocha huyo anatarajia kuondoka nchini leo Ijumaa kuelekea Cameroon kwa ajili ya kwenda mapumziko na familia yake, lakini akadai kuwa atakapokuwa huko atakuwa na kazi ya kuangalia wachezaji na iwapo atamuona anayefaa, basi atautaarifu uongozi ili kuweza kufanyia kazi.

“Kwa sasa kila mtu yupo mapumziko kuanzia kocha, wachezaji hadi uongozi baada ya kumaliza ligi, tutajiandaa kuhakikisha tunafanya usajili wa kiwango cha juu kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa Afrika na si ligi kuu pekee.

“Kila mmoja amepewa jukumu lake kuelekea usajili wa msimu ujao lakini kwa sasa ni mapema mno kuweza kuweka wazi juu ya kinachoendelea, tusubiri kwanza,” alisema Nassoro.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic