April 4, 2014





Kutokana na mwenendo wa kusuasua wa Simba katika Ligi Kuu Bara, beki wa kati wa timu hiyo, Joseph Owino, raia wa Uganda, amekiri kwa kusema kwamba hawana chao msimu huu, hivyo wanaziachia Simba, Yanga, Azam na Mbeya City zipambane zenyewe kwenye tatu bora.


Owino ambaye amekuwa nahodha wa mechi kadhaa baada ya Said Nassor ‘Chollo’ kuwekwa benchi huku Amri Kiemba akiwa na matatizo ya kifamilia, alisema kwamba ni kama wamepitiwa na upepo mbaya, hivyo ni bora wakamilishe ratiba, ligi imalizike waanze upya msimu ujao.

Alisema kwamba kwa hali jinsi ilivyo ni vigumu kuwaahidi mashabiki kwamba watafika nafasi ipi kabla ya ligi kuisha kutokana na ushindani na kasi iliyopo baina ya Mbeya City, Yanga na Azam kwenye nafasi za juu msimu huu.

“Ukiangalia timu yetu ni nzuri tu wala si mbovu lakini ni kama upepo mbaya umetupiga msimu huu, kwa hiyo ngoja tukamilishe ratiba ligi imalizike, tuanze upya kwa nguvu mpya.

“Mechi nyingi huwa tunacheza sisi mpira lakini utashangaa baadaye ndiyo tunafungwa au tunatoka sare, kwa jinsi hali ilivyo ni ngumu kusema kwamba tutafika nafasi fulani, msimu huu tuwaache tu Yanga, Azam na Mbeya City ambao wanaonekana wapo vizuri waendelee kupambana,” alisema Owino.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic