Rais wa TFF, Jamal Malinzi amekubali kuwa
kuna mchezo mchafu wa baadhi ya waamuzi kuchukua rushwa.
Malinzi amesema kuna waamuzi ambao si
waaminifu wanaofanya mchezo huo mchafu lakini akasisitiza, siku itafika tu.
“Kweli si kitu kizuri na kinaturudisha
nyuma, lakini siku itafika tu. Nikimkamata mtu, atakuwa mfano kwa wengine, wewe
ngoja tu,” alisema Malinzi wakati akifanya mahojiano na Radio One.
Baadhi ya waamuzi wamekuwa wakishutumiwa
kuchukua mlungula kutoka kwa baadhi ya klabu na kuzisaidia.
Hata hivyo, baadhi ya waamuzi wamekuwa
wakipinga na maofisa wengine wakidai suala hilo ni kama kuwachafua.
Lakini kitendo cha Rais wa TFF
kulikubali hadharani na kutangaza vita kwa wanaohusika, huenda ikawa ni sehemu
ya dawa.
0 COMMENTS:
Post a Comment