April 4, 2014

NETO AKIFURAHIA BAADA YA MGAMBO KUILAZA YANGA

Yanga imekata rufaa kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ikipinga usajili wa Mohammed NEto wa Mgambo.

Katika rufaa ya Yanga kwenda TFF imeeleza kuwa Neto ni raia wa kigeni lakini amesajiliwa kama raia wa Tanzania.
Kutokana na hatua hiyo, Yanga imetaka kurudishiwa pointi tatu ilizozipata Mgambo baada ya kuwafunga mabingwa hao mabao 2-1 mjini Tanga, wiki iliyopita.
Neto alicheza kwa dakika 32 na kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kuelezwa kuwa alikuwa na hirizi.
Lakini siku moja baadaye akaibuka na kusema hakuwa na hirizi wala kitu cha ncha kali kama ilivyoelezwa, lakini kumekuwa na wachezaji wakubwa wanaocheza na hirizi lakini hawaripotiwi.
Yanga inachuana na Azam FC kileleni kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara na kama itapewa pointi hizo tatu, itakuwa imezidi kunogesha mbio za ubingwa huo.

Azam FC inaongoza ikiwa na pointi 53 katika mechi 23 ilizocheza na Yanga ni ya pili ikiwa na pointi 46 katika mechi 22.

1 COMMENTS:

  1. Mfa maji haachi kutapatapa kwani yanga hawakiliona hili mzunguko wa kwanza waliposhinda bao 3 bila mbona yanga wanataka walete uhuni na pia mchezaji aliposajiliwa c kulikuwa na mda wa kuweka pingamizi mda huo yanga walikuwepo wapi wasiweke pingamizi ? Mpira wa bongo bwana magumashi kibao, bila shaka wameshapew mchongo na baadh ya viongozi wa TFF wenye mapenz na yanga

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic