Uongozi wa Yanga umesema kiungo
mshambuliaji wake, Emmanuel Okwi anasumbuliwa na maumivu ya enka.
Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu amesema
pamoja na kuzagaa kwa taarifa mbalimbali, lakini Okwi ni mgonjwa.
“Mambo mengi sana yameelezwa, lakini
ukweli Okwi ni mgonjwa na hakuna suala lingine.
“Unajua wanasema maneno ya kila namna,
lakini alikuwa anasumbuliwa na enka. Hata wakati anakwenda Tanga alikuwa na
maumivu makali sana,” alisema Njovu.
Taarifa zilizopo, zinaeleza Okwi anaidai
Yanga dola 40,000 ambazo hakumaliziwa kwenye usajili wake uliogharimu zaidi ya
dola 100,000 ndiyo maana amekuwa akisusia mazoezi.
Siku nzima leo, simu ya Okwi ilikuwa
inaita bila ya kupolekewa lakini kuna taarifa zimeeleza kuwa amekuwa hapokei
hata simu za viongozi wa Yanga.
Lakini Njovu akasisitiza wamekuwa
wakiwasiliana na Okwi bila ya matatizo na wanajua kinachombua na hasa ni suala
la maumivu na si vinginevyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment