June 30, 2014



Mgombea aliyeenguliwa katika kiti cha urais wa Simba, Michael Richard Wambura, amekumbana na kizingiti kingine katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo, jana Jumapili.


Katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay jijini Dar, Wambura alizuiwa getini wakati akiwa kwenye foleni akijiandaa kuingia ndani ya ukumbi.

Mara baada ya kuzuiwa, Wambura alisema amezuiwa kutokana na jina lake kutotokea katika orodha ya wanachama wa klabu hiyo, hivyo anashangaa kitendo hicho kilichotokea ambacho siyo sahihi huku akidai kuwa yeye ni mwanachama halali wa Simba.

“Kiukweli nasikitika sana kwa kitendo hiki kilichotokea cha kuzuiwa mlangoni wakati najiandaa kuingia kwenye ukumbi wa kupigia kura, eti wanasema jina langu halionekani katika mtandao.

“Mimi sina jinsi, nimeona ni bora niondoke zangu, lakini ninaendelea kuchunguza kujua kilichotokea, mimi ninajua ni mwanachama halali wa Simba,” alisema Wambura akionyesha kusikitishwa na jambo hilo.
Awali Wambura alienguliwa kushiriki uchaguzi huo baada ya kujitokeza akiwania nafasi ya urais na mwisho wanachama wakatinga mahakamani lakini pia wakashindwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic