June 2, 2014



Uongozi wa Mbeya City umesema hauna sababu ya kuwalaumu wachezaji kwa kutupwa nje ya michuano ya Kombe la Nile Basin, kwa kile walichosema kuwa kwa kiwango chao, kufika robo fainali ni hatua kubwa mno.

Mbeya City ambao ndiyo walikuwa wawakilishi pekee wa Tanzania Bara, wanatarajiwa kutua nchini leo asubuhi wakitokea mjini Khartoum, Sudan baada ya kutupwa nje na timu ya Victoria ya Uganda kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0 katika mchezo wa robo fainali juzi.

Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Mbeya City kushiriki michuano ya kimataifa, tangu kuanzishwa kwake miaka mitatu iliyopita.

Akizungumza kutoka Sudan, Msemaji wa timu hiyo Freddy Jackson, alisema kuwa wanatarajia kuwasili nchini leo asubuhi au alfajiri sana, lakini hii yote itategemeana na ratiba ya ndege.
Aidha Jackson, alisema licha ya kutupwa nje kocha Juma  Mwambusi na jopo zima la timu hiyo, halina cha kulaumu bali kujivunia kutokana na kupata changamoto na imewapa uzoefu wa kutosha wachezaji wao.
“Sawa kila timu ina ndoto ya kutwaa ubingwa na sisi ndiyo ilikuwa ‘tageti’ yetu, lakini ndiyo hivyo tumetolewa. Hatuwezi kulaumu sana na lazima tujivunie kufika robo fainali kwa timu kama Mbeya City ambayo ndiyo kwanza ilinusa michuano hii.
“Kuna kitu tumejifunza, wachezaji wetu wamepata uzoefu fulani ambao utatusaidia katika ligi kuu msimu unaoanza,” alisema Jackson.
Aliongeza kuwa, huenda wasivunje kambi baada ya kufika huku, au wakatoa likizo ya wiki moja ya mapumziko kabla ya kuendelea ya kambi kwa ajili ya maandalizi ya ligi kuu bara.
Tayari Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetanmgaza tarehe ya kuanza kwa ligi kuu ambayo itaanza kurindima Agosti 24, mwaka huu.

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic