June 2, 2014



Kiungo nyota wa UiTM FC, inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Malaysia, Mtanzania, Abdi Kassim ‘Babi’, amesema tatizo ambalo linawafanya wachezaji wa Kibongo washindwe kucheza soka la kulipwa ni kukosekana kwa chips mayai sehemu ambazo wanatakiwa kwenda kucheza.


Babi ambaye alisaini mkataba wa mwaka mmoja, amepata mafanikio ya kupewa unahodha kwa muda mfupi tangu alipojiunga na kikosi hicho mapema mwaka huu.
Akizungumza na SALEHJEMBE moja kwa moja kutoka Malaysia, Babi alisema anashangazwa na kitendo cha wachezaji wa Kibongo kukataa ofa za kucheza soka la kulipwa na anahisi labda tatizo kubwa ni huko waendako hakuna chips mayai, hali inayosababisha waamue kukataa kwa kuwa wamezoea chakula hicho.
Alisema mtu mwenye malengo siku zote hawezi kushindwa kuyatafuta lakini anawashangaa wachezaji wengi wa Kibongo jinsi wanavyolichukulia soka.
“Inawezekana wakawa ‘wanamis’ chips mayai wanapokuwa nje ya Bongo au familia lakini mtu mwenye malengo hawezi kushindwa, mimi huku nacheza vizuri na wala hakuna hizo chips,” alisema Babi na kuongeza:
“Soka la huku lina ushindani mkubwa sana, tena kuliko hata la huko Bongo.”

Babi ni kiungo anayesifika kwa kupiga mashuti na kontroo ya mpira na alipata umaarufu mkubwa wakati akiichezea Yanga takribani miaka miwili iliyopita

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic