Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij amegoma kujibu swali
kuhusiana na uamuzi wa kumrejesha Mrisho Ngassa kwenye kikosi chake na
kusisitiza anapaswa kujibu mwenyewe.
“Siwezi kujibu, yuko hotelini. Mnaweza kumtafuta na
kumuuliza kwa nini ilikuwa hivyo,” alisema Nooij.
Taifa Stars tayari ipo kambini kujiandaa na mechi dhidi ya Msumbuji kuwania kufuzu kwenye michuano ya Kombe la Mataifa Afrika.
Awali Yanga ilihoji kuhusiana na Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) kumruhusu Ngassa kwenda kufanya majaribio Afrika Kusini bila ya
ruhusa ya klabu ambayo ilikuwa inajua yuko kambini Botswana.
Lakini Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Celestine akasema
Ngassa hakuripoti kambini tokea siku ya kwanza, hivyo TFF haijui lolote na
Nooij aliamua kumuondoa na angeikosa mechi ya Msumbuji.
Lakini sasa kila mmoja amekuwa akiruka kuhusiana na
suala na tayari Ngassa ameanza kujifua na Stars tayari kuivaa Msumbuji.
0 COMMENTS:
Post a Comment