Mshambuliaji mpya wa Barcelona, Luis Suarez
ametua katika klabu yake hiyo mpya kukamilisha dili la pauni milioni 75
akitokea Liverpool.
Lakini Fifa imeweka msisitizo kwamba Barcelona
haitatakiwa kumtambulisha Suarez katika kipindi chote cha miezi minne
alichofungiwa.
Suarez alifungiwa kutokana na kumng’ata beki
Giorgio Chiellini wa Italia wakati wa michuano ya Kombe la Dunia.
Tayari jezi za Suarez aliyekuwa mfungaji bora
Ligi Kuu England zimeanza kuuzwa mgongoni zikiwa na namba 9 iliyokuwa inavaliwa
na Alexis Sanches ambaye amejiunga na Arsenal.











0 COMMENTS:
Post a Comment