![]() |
| MWAKIBINGA (KUSHOTO) AKIWA NA MKURUGENZI WA AZAM TV, TORRINGTON, SIKU WALIPOINGIA MKATABA WA KUONYESHA LIVE LIGI KUU BARA. |
Licha ya uongozi wa Yanga kuendelea kushikilia
msimamo wake kukataa milioni 100 za udhamini kutoka Azam TV, Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), limesema kuwa hiyo haitawazuia kuonyesha mechi zao za msimu
mpya.
Ofisa Mtendaji wa Bodi ya Ligi, Silas
Mwakibinga, amesema pamoja na Yanga kususia kitita hicho, ni lazima mechi zao
ziwe live kwa mujibu wa mkataba na mdhamini.
“Fedha zao zipo benki zimetunzwa, kama
unavyojua tayari AzamTV wametoa mgawo wa awali, wao hawajachukua kama
walivyosusia msimu uliopita.
“Lakini hiyo haimkatazi mdhamini kuonyesha
mechi zao msimu huu na nikuhakikishie lazima mechi zote zirushwe ‘live,”
alisema bosi huyo.
Msimu uliopita, Yanga walikataa kuchukua
milioni 100 kwa kile walichodai kuwa ni kiasi kidogo na kwamba hawawezi
kuchukua kiasi sawa na timu ndogo.








0 COMMENTS:
Post a Comment