August 6, 2014


LUIZIO


Wakati Simba ikiwa katika maandalizi yake  kuelekea Simba Day, siku ya Jumamosi ambapo itavaana na Zesco ya Zambia, Mtanzania amewapa onyo.


Aliyekuwa mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Juma Luizio, amefunguka kuwa Simba lazima wajipange kutokana na timu hiyo kuwa vizuri kisoka, hivyo lolote linaweza kutokea.

Simba inatarajia kukutana na Zesco Agosti 9, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa katika mchezo wa kirafiki ambapo timu hiyo itakuwa inaadhimisha siku yake maalum ya kuwatambulisha wachezaji wake wapya.

Akizungumza kutoka nchini Zambia, straika huyo alisema timu yake hiyo mpya ipo vizuri sana, hivyo Simba wanapokutana nao ni lazima waje kwa tahadhari kubwa.

“Zesco itavaana na Simba Jumamosi, lakini napenda kusema wajipange tu kwa sababu timu hii ipo vizuri, wanatakiwa kuja na tahadhari kubwa sana, kama unavyofahamu kwenye soka lolote linaweza kutokea.
“Kwa sababu timu hii ina wachezaji wengi wazuri kutoka nje, ndiyo maana inafanya vyema, japo mpira siku zote hautabiriki, kikubwa tu wao wajipange na mimi naifahamu timu hiyo pia,” alisema Luizio.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic