Mohammed Salim, Pemba
Kikosi cha Yanga kimewasili mjini
Pemba kwa ajili ya kambi maalum kwa maandalizi ya Ligi Kuu Bara msimu ujao.
Yanga wametua visiwani hapa, lakini si
kikosi kizima.
Wametua kwa mafungu kwa madai ni
kutokana na suala la usafiri wa ndege.
Mmoja wa viongozi amesema kuwa fungu
jingine la wachezaji litawasili baadaye leo.
Yanga itakuwa hapa Pemba kwa takribani
wiki tatu chini ya Kocha Marcio Maximo kujiandaa na Ligi Kuu Bara iliyopangwa
kuanza Septemba 20.
Kabla ya hapo, Yanga ilikuwa ikijifua
jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuanza maandalizi hayo.
0 COMMENTS:
Post a Comment