September 1, 2014



Mkurugenzi wa wa Vyama na Masuala ya Kisheria katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Evodius Mtawala, amelazimika kuachia ngazi kutokana na sababu mbalimbali.


Taarifa ambazo tumezipata, zinaeleza kuwa Mtawala ambaye aliwahi kuwa  Katibu Mkuu wa Simba, alikuwa na hali ya kutokuelewana na uongozi wa shirikisho hilo na ndiyo chanzo kikubwa cha kumfanya ang'atuke TFF.

Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa, alithibitisha kuachia ngazi kwa Mtawala lakini akasema ni kutokana na sababu mbalimbali za taaluma yake ya uanasheria.

“Ni kweli Mtawala hataendelea kufanya kazi TFF lakini ameamua kuchia ngazi mwenyewe kutokana na sababu mbalimbali alizodai kwamba ni kujikita na taaluma yake zaidi kwa sasa, lakini mambo mengine juu ya hilo yatabaki kuwa siri baina yake na mwajiri wake.

“Ila mpaka makubaliano ya mwisho yalieleza kuwa itakapofika mwisho wa mwezi wa nane (jana 31, Agosti) atakuwa tayari ameshakabidhi ofisi na kuendelea na masuala ambayo alidai anahitaji kujikita zaidi kulingana na taaluma yake,” alisema Mwesigwa.

Mtawala amedumu kwenye wadhifa huo kwa miezi nane tu tangu alipoteuliwa Desemba 24, mwaka jana chini ya uongozi wa rais mpya, Jamal Malinzi. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic