September 24, 2014

GLOBAL FC...
Timu ya Global FC ambayo imeshinda mechi nne mfululizo za kirafiki, leo Jumatano inatarajiwa kujitupa uwanjani kupambana na timu ya Wizara ya Katiba na Sheria katika mchezo wa kirafiki utakaopigwa kwenye Uwanja Mawasiliano, Ubungo jijini Dar.

Mkurugunzi wa Habari na Mawasiliano wa Global FC, Nassor Gallu,amesema mbali na mchezo huo wa soka, pia kutakuwa na michezo mingine ikiwemo kuvuta kamba baina ya timu hizo, lengo likiwa ni kuboresha uhusiano na kuimarisha afya.
“Siku ya Jumatano (leo) tutakuwa na mchezo wa kirafiki dhidi ya wenzetu wa Wizara ya Katiba ambao wanajiandaa na mashindano ya Shimiwi. Lakini jambo jema ni kwamba mbali na soka, pia kutakuwa na mchezo wa kuvuta kamba.
“Lengo ni kujiimarisha kiafya na kuboresha uhusiano maana michezo ni furaha. Kikosi chetu kipo vizuri, kwa hiyo niwaomba mashabiki waje kwa wingi kushuhudia burudani hiyo,” alisema Gallu.

Timu ya Global imekuwa ikicheza mara kwa mara michezo ya kirafiki ambapo Ijumaa ya wiki iliyopita, ilikipiga na Shein Rangers na kutoka nao suluhu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic