September 29, 2014


Simba imepata pigo jingine baada ya beki wake wa pembeni mkongwe, Nassor Said ‘Chollo’ kuumia mkono wa kulia wakati timu yake ilipocheza dhidi ya Polisi Morogoro juzi, hivyo kuna uwezekano wa kuikosa mechi dhidi ya Yanga.

Tayari Mkenya, Paul Kiongera na kipa Ivo Mapunda wataikosa Yanga kutokana na majeraha. Simba itakutana na Yanga Oktoba 18 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Vipimo vya madaktari atakavyofanyiwa leo, ndiyo vitaamua hatma yake ya kuikosa mechi ya Yanga.
Chollo alipoumia juzi, alilazimika kufungwa bandeji na kutolewa nje na nafasi yake kuchukuliwa na William Lucian ‘Gallas’.

Daktari Mkuu wa Simba, Yassin Gembe, alisema hatima ya beki huyo itajulikana baada ya vipimo vya mwisho atakavyovifanya leo kwenye Hospitali ya Mkoa wa Temeke.
Gembe alisema, bado haijulikani beki huyo amepata tatizo gani kwenye mkono huo wa kulia kama ameteguka au kuvunjika, hivyo hatima yake itajulikana leo.
 “Hivi sasa anaendelea kupata matibabu ya timu kutoka kwangu na kesho nitampeleka kwenye Hospitali ya Mkoa wa Temeke kwa ajili ya vipimo zaidi ili kujua amepata majeraha gani kabla ya kutoa tamko rasmi kuwa atakuwa nje ya uwanja muda gani,” alisema Gembe.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic