September 10, 2014


Kipa namba moja wa Simba, Ivo Mapunda amemuonya kiungo wao mshambuliaji, Mganda, Emmanuel Okwi, kuwa asiwajibu na wala kuwafikiria mashabiki wa Yanga kila wanapomzomea akiwa ndani na nje ya uwanja.

Ivo ambaye amewahi kuichezea Yanga, aliitoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache tangu itangazwe rasmi na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwa Okwi yupo huru kuichezea Simba.
Okwi, hivi karibuni alisaini mkataba wa miezi sita ya kuichezea Simba kabla ya Yanga kumshtaki TFF ikitaka imlipe fedha za usajili ilizompa huku ikimuondoa kwenye usajili wa msimu ujao.
Ivo amesema zomeazomea ya Yanga isimchanganye kabisa Okwi, kikubwa anachotakiwa ni kufanya kazi yake ndani ya uwanja.
Ivo alisema Yanga wanafanya kitendo hicho kwa ajili ya kumchanganya kisaikolojia ili asicheze soka, sasa yeye akizisikiliza kelele zao basi soka litamshinda.
 “Katika maisha siyo kila mtu anakupenda, ni vyema kwanza Okwi akalifahamu hilo, anachotakiwa kukifanya ni kuachana na mashabiki wa Yanga pale wanapomzomea anapokuwa uwanjani kwa kuweka pamba masikioni na kucheza soka.
“Lakini kama akitaka kujibizana nao, basi hatacheza soka tena na asipoangalia atashusha kiwango chake, mimi niliongea kabla ya mechi ya kirafiki na Gor Mahia nikijua lazima hali hiyo itatokea,” alisema Ivo.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic