September 7, 2014


Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imeanza kusikiliza kesi inayomhusu mshambuliaji Emmanuel Okwi.
Kesi hilo inasikilizwa kwenye hoteli ya kitalii ya Colosseum ya jijini Dar es Salaam.

Habari zinaeleza kuwa kuna mvutano mkali wa kisheria kuhusiana na kesi hiyo ambayo Yanga na Simba zinamgombea Okwi raia wa Uganda.
Yanga inaeleza bado ni mchezaji wake na ina mkataba naye ingawa imemfungulia madai TFF ikitaka kuvunja naye mkataba na afungiwe, pia alipe kitita cha faini ya Sh milioni 700. Kati ya hizo milioni 200 kwa ajili ya kuzungumza na timu ya Misri akijua ana mkataba na milioni 500 kuingia mkataba na Simba wakati akijua ana mkataba na Yanga.
Lakini Simba imemsainisha mkataba wa miezi sita kwa kuwa ameomba imsitili kipaji chake kwa kuwa Yanga imeandika barua ya kuvunja mkataba naye akasema sawa.

Kesi hiyo ndiyo inaendelea sasa na huenda leo majibu yakapatikana kama ukali wa mvutano hautazidi kupanda juu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic