September 17, 2014

BENZEMA AKIPACHIKA BAO LA 1000...
Klabu ya Real Madrid imekuwa ya kwanza kufunga mabao 1000 katika michuano ya Ulaya.

Mshambuliaji wake Karim Benzema raia wa Ufaransa ndiye aliyefunga bao hio la 1000 wakati Madrid ikishinda mabao 5-1 dhidi ya Basle ya Uswiss katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi.
Benzema ameingia kwenye rekodi za klabu hiyo kwani wa mwisho alikuwa ni Cristiano Ronaldo ambaye alifunga bao la 900 mwaka 2011 wakati Madrid ikiibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Lyon.
Mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo, Roberto Soldado ndiye alifunga bao la 800 akiunganisha krosi ya David Beckham.
Lakini kabla ya Soldado, mshambuliaji nyota zaidi wa klabu hizo enzi hizo, Raul Gonzalez ndiye alipata rekodi ya kufunga bao la 700.

Alifunga bao hilo siku ambayo alikuwa ameweka rekodi ya kufikisha mabao 71 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic