October 9, 2014

 Simba imeendelea na mazoezi leo kujiandaa na mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya watani wake Yanga, Oktiba 18 jijini Dar es Salaam.

Mazoezi hayo ni sehemu ya kujiweka vizuri kabla ya mechi yake ya kwanza ya kirafiki dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
Mechi hiyo itakayopigwa kwenye kitongoji chenye weusi wengi cha Soweto jijini Johannesburg, itakuwa ni ya kwanza kwa Simba.
Taarifa zinaeleza Simba itacheza mechi mbili ingawa keshokutwa Jumamosi, itawakosa wachezaji wake walio katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars ambayo itakuwa inacheza na Beni jijini Dar.
Wachezaji wake walio Stars ni Joram Mgeveke, Jonas Mkude, Said Ndemla, Amri Kiemba na Haruna Chanongo ambao watatua Johannsburg maarufu kama Jozi, Jumatatu.
Simba pia itamkosa Okwi ambaye atabaki Kampala, Uganda akiitumikia timu yake ya taifa inayotafuta nafasi ya kucheza Kombe la Mataifa Afrika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic